Hivi ndivyo Barca ilivyomegwa vipande si mchezoooo.....
22:27
KLABU ya Bayern Munich wameanza vyema
kampeni ya kuelekea kucheza fainali ya tatu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
ndani ya miaka minne, baada ya kuikung'uta Barcelona mabao 4-0 usiku
huu kwenye Uwanja wa Allianz Arena katika Nusu Fainali ya kwanza.
Mabao mawili kutoka kwa Thomas Muller na
moja kwa kila mmoja, Mario Gomez na Arjen Robben yamempa faraja kocha
Jupp Heynckes ambaye sasa sijui itokee miujiza gani Jumatano ijayo
Uwanja Nou Camp kwenye mchezo wa marudiano akose tiketi ya kwenda
Wembley.
Kikosi cha Bayern Munich kilichofanya
mauaji hayo kilikuwa: Neuer, Lahm, Boateng, Dante, Alaba, Javi Martinez,
Schweinsteiger, Robben, Muller/Pizarro dk83, Ribery/Shaqiri dk88 na
Gomez/Gustavo dk71.
Barcelona: Valdes, Dani Alves, Pique, Bartra, Jordi Alba, Xavi, Busquets, Iniesta, Sanchez, Messi na Pedro/Villa dk83.
0 comments:
Post a Comment