Hivi ndivyo Barca ilivyomegwa vipande si mchezoooo.....

KLABU ya Bayern Munich wameanza vyema kampeni ya kuelekea kucheza fainali ya tatu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ndani ya miaka minne, baada ya kuikung'uta  Barcelona mabao 4-0 usiku huu kwenye Uwanja wa Allianz Arena katika Nusu Fainali ya kwanza.
Mabao mawili kutoka kwa Thomas Muller na moja kwa kila mmoja, Mario Gomez na Arjen Robben yamempa faraja kocha Jupp Heynckes ambaye sasa sijui itokee miujiza gani Jumatano ijayo Uwanja Nou Camp kwenye mchezo wa marudiano akose tiketi ya kwenda Wembley.
Kikosi cha Bayern Munich kilichofanya mauaji hayo kilikuwa: Neuer, Lahm, Boateng, Dante, Alaba, Javi Martinez, Schweinsteiger, Robben, Muller/Pizarro dk83, Ribery/Shaqiri dk88 na Gomez/Gustavo dk71.
Barcelona: Valdes, Dani Alves, Pique, Bartra, Jordi Alba, Xavi, Busquets, Iniesta, Sanchez, Messi na Pedro/Villa dk83.