MTUMISHI WA WIZARA YA ELIMU ANASWA AKIWA GESTI NA MUME WA MTU

Tukio hilo la kuchafua sifa ya ndoa, lilijiri hivi karibuni mjini Morogoro ambako Rose(mke wa Kanali Mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ) aliaga kwa mumewe anakwenda kikazi.
Kapu la habari lililosheheni picha za video  liliwasilishwa mbele ya gazeti moja maarufu hapa nchini  hivi karibuni na mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Sarah huku maelezo yakimtuhumu Rose kujivinjari na mumewe katika faragha haramu.


Habari   zilieleza kwamba, mtumishi huyo wa wizara  alidaiwa kuingilia ndoa ya mtu kwa kutumia safari zake za kikazi kula nyama ya ulimi na mume wa mtu huyo aliyetajwa kwa jina moja la Kesi ambaye hatimaye alinaswa naye.

 “Kuna watu waliniambia kuwa, Kesi ambaye ni mume wangu anatembea na mwanamke huyo, nikaanza kufuatilia hatua kwa hatua kwa kuwatumia watu wakiwemo watumishi wa hoteli aliyofikia Rose na mume wangu.
“Sikupenda kuwaingilia chumbani na kuwaharibia starehe zao, nilichotaka mimi ni ushahidi, nilitumia ujanja wangu kupenyeza kamera nikapata picha,” alisema Sarah huku akifungua kompyuta mpakato yake (laptop) na kuonesha tukio zima mbele ya ofisi ya gazeti hilo.

Katika kulithibitisha tukio,mtumishi huyu wa Wizara ya  Elimu  alipigiwa simu na maongezi yakawa kama ifuatavyo

Mwandishi: Habari yako dada Rose?
Rose: Nzuri, naongea na nani?
Mwandishi: Naitwa (tunalihifadhi) ni mwandishi wa Gazeti la Ijumaa.


Rose: Ndiyo, unasemaje?
Mwandishi: Aaa, hapa kuna tuhuma zako kwamba unatembea na mume wa mtu na kwamba hivi karibuni ulikuwa naye ndani ya gesti moja mjini Morogoro, lakini pia zipo picha za video na mnato zikionesha mambo machafu mliyoyafanya huko, sijui unajua chochote kuhusu hili?


Rose: We uko wapi, …kama ni ofisini nakuja sasa hivi kuziona hizo picha, nitakujibu nikifika.

Bila kuchelewa, dakika 27 baadaye Rose  alifika katika ofisi za Ijumaa  akiwa na mumewe  na waliomba  kuziona picha, jambo ambalo liliwapa wakati mgumu wahariri kukubali zoezi hilo lifanyike mbele ya mwanaume huyo.

“Sikiliza kijana, huyu ni mke wangu, sasa unataka kuficha nini, umempigia simu, kaniambia, sisi tukakubaliana tuje wote kama mwili mmoja, sasa wewe unakataa nini…au ulikuwa na mambo yako?” alihoji kwa ukali mume wa mwanamke huyo.

Wahariri hatimaye walikubaliana na  ombi la wanandoa hao kuona picha hizo kwa pamoja, hivyo walipelekwa kwenye kompyuta na kuanza kufunguliwa kifurushi kimoja baada ya kingine .

“Mume wangu tulikuwa tumekaa tu hapa, huyu kaka alikuja kunitembelea chumbani, umeona nimevua nguo? Rose alijitetea kwa mumewe baada ya kifurushi cha kwanza kufunguliwa na kuwaonesha wakiwa wamekaa kitandani na jamaa.
 Kauli hiyo ya mtumishi huyo wa umma mbele ya mumewe ilikuwa kama kutia nazi kwenye supu kwani kimsingi video iliwaonesha wawili hao wakishirikiana ipasavyo hali iliyomfanya mumewe ashushe pumzi.

Mpaka mwisho wa sinema hiyo yenye dakika chache lakini zenye ‘machungu’, wanandoa hao waliondoka wakiwa ‘wamelowa’ jasho

HABARI HII IMEANDALIWA KWA HISANI YA MAGAZETI PENDWA YA GLOBAL PUBLISHER .JIPATIE NAKALA YAKO LEO