Muuza Bangi amchoma Kisu Polisi


KIJANA mmoja mkazi wa Kurasini jijini Dar, Francis Huruma maarufu kwa jina la Big anayedaiwa kuuza madawa ya kulevya aina ya bangi, amemchinja polisi mwenye namba H.617 Anthony Pasco (22).
Tukio hilo la aina yake lilitokea hivi karibuni katika Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Ugimbi uliopo Kurasini, Dar.
Mbali na kumchinja kwa kisu polisi huyo shingoni na kutofanikiwa kumuua kama alivyokusudia, Big pia alimjeruhi vibaya polisi mwingine mwenye namba H.334 Akili Mlawa (23) kwa kisu mguuni na mkononi.
Polisi wote waliopatwa na majeraha wamelazwa katika Hospitali ya Jeshi la Polisi, Kilwa Road, jijini Dar.
Raia walioshuhudia tukio hilo, walimvamia Big kisha wakamshushia kipigo na baadaye akafariki dunia wakati akitibiwa katika Hospitali ya Temeke, Dar.