GERALD HANDO- wa Clouds FM nusura afumuliwe na Bastola leo

MTANGAZAJI maarufu wa Clouds FM, Gerald Hando leo alfajiri alizua kizaazaa na kupelekea kutishiwa bastola na mtu ambaye jina lake halikufahamika mara moja.
Chanzo cha Saluti5 kimesema Hando aligonga gari la mtu huyo maeneo ya Kwa Kopa, jambo lililopelekea mtu huyo ashuke kwenye gari lake bastola ikiwa mkononi na kutishia kumfumua Hando.
Kama mtu huyo alidhani kutoa bastola ndio suluhisho basi alikosea sana, Gerald Hando anayetangaza kipindi cha "Power Breakfast" naye alishuka kwenye gari lake na kufungua shati lake na kuanza kumuamrisha mtu huyo afyatue bastola.
Huku akiporomosha matusi kwa ukali Hando alisema: “Piga hiyo bastola yako, shoot me.”
Hando aliendelea kuwa mkali huku akipigapiga kifua chake hali iliyovuta watu wengi kwenye tukio hilo ambao waliwasihi wote wawili kutuliza mzuka na kumfanya mtu huyo aliyekuwa na gari aina ya Rav 4 arudishe bastola yake kwenye gari na kutafuta njia nyingine ya kulimaliza tatizo lililotokea.
TOA MAONI YAKO HAPA