Baada Ya Fungate 2face Sasa Kuendelea Na Shuguli Zake Kama Kawaida..

Baada ya kufunga ndoa na mkewe Annie Idibia iliyofana nchini Dubai, msanii 2face Idibia ambaye hivi karibuni amewasili nyumbani Nigeria tayari ameanza kujipanga upya kwa ziara kubwa iliyobatizwa jina ‘Africa All-Star tour’ inayotarajiwa kuanza tarehe 13 mwezi huu jijini Lagos.
Ziara hiyo inatarajia kuwashwa moto na wasanii wakali nchini Nigeria wakiwemo 2face mwenyewe, Davido, Ice Prince na Professor.
Dhumuni haswa la ziara hiyo iliyoandaliwa na taasisi moja ya burudani ni kuendeleza kampeni ya kukuza na kusambaza muziki wa kiafrika na vilevile kutangaza zaidi vipaji vya muziki vinavyopatikana barani Afrika.
Aidha, tamasha la ziara hiyo litafanyika nchini Durban, na Afrika Kusini Mei 18 mwaka huu ambapo mkali wa michano Snoop Lion aka Snoop Dogg, atahitimisha tamasha la ziara hiyo huko Durban.