Tanzania haipo kwenye orodha ya nchi ishirini masikini duniani

Nimeiona orodha ya nchi 20 masikini zaidi dunia na jambo la kufurahisha ni kuwa tanzania haipo kwenye orodha hiyo.nchi ya msumbiji ipo kwenye orodha ya nchi masikini lakini kuna jambo limenishangaza kidogo.thamani ya pesa ya msumbiji iko juu zaidi na ya kwetu kwa maana kwasasahivi 1000tsh = 18.97 meticais.sasa wale ndugu zangu wataalamu wa uchumi naomba mnisaidie kuhusu hili.kwa upeo wangu mdogo thamani ya pesa ya nchi fulani yaweza kutumika kama kigezo cha kubaini hali na kiwango cha uchumi wa nchi fulani?najua zipo sababu zingine kadhaa lakini hili limenishangaza kwa kiasi fulani
Read more Here:http://www.therichest.org/world/poorest-countries-in-the-world/
TOA MAONI YAKO HAPA