MREMBO DIANA LAIZER ANYAKUWA TAJI LA MISS MOROGORO

 
Miss Morogoro 2013, Diana Laizer (21) katika pozi baada ya kutwaa taji hilo.
Mrembo Diana Laizer (21) usiku wa kuamkia leo ametwaa taji la Miss Morogoro 2013 kwenye shindano lililokuwa na upinzani mkali lililoshuhudiwa na umati mkubwa wa watu wakiongozwa na mgeni rasmi, Waziri wa Fedha Mstaafu, Mustapha Mkulo, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kilosa mkoani Morogoro.
Shindano hilo lilishirikisha warembo 10 kutoka wilaya zote za mkoa wa Morogoro. Mshindi wa pili katika kinyang'anyiro hicho ni Sabra lsmail wakati nafasi ya tatu ikienda kwa Muzne Abduly.