Ripoti ya Polisi yamsafisha RC Mulongo dhidi ya Lema
22:21
Kamanda wa
Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, amedai uchunguzi wa awali
kuhusu ujumbe unaodaiwa kutumwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa
Mulongo(pichani), umetumwa na mtandao wa simu wa nje ya nchi. Kamanda
alisema katika ujumbe huo ambao Lema anadai uliandikwa na Mkuu wa Mkoa
Mulongo na kutumwa kwenye simu yake Aprili mwaka huu, uchunguzi wa
polisi umeonyesha kwamba haukutumwa kupitia kampuni moja wapo ya simu za
mikononi ya hapa nchini.
“Katika
kipindi cha mwishoni mwa Aprili mwaka huu, vyombo vya habari viliandika
na kutangaza habari iliyoelezea shutuma zilizotolewa na Mbunge Lema
kuwa aliandikiwa ujumbe wa vitisho kwa njia ya simu na Mkuu wa Mkoa
Mulongo na ulisomeka: “Umeruka kihunzi cha kwanza nitakuonyesha mimi ni
serikali, ulikojificha nitakupata na nitakupa kesi inayoitaka mimi.”
Sabas alisema ujumbe huo ulidaiwa kutumwa kutoka namba 0752960276
inayotumiwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo kwenda kwenye namba 0764150747
inayotumiwa na Lema.
Alisema kufuatia tuhuma hizo, polisi walianza uchunguzi kwa kuzingatia
kuwa Mulongo alikanusha kutuma ujumbe wa aina yo yote kwa Lema.
Alisema uchunguzi huo ulihusisha kampuni ya simu ambayo mtandao wake ulitumika katika utumaji wa ujumbe husika.
Alisema uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa chanzo cha ujumbe huo
mfupi hakikuwa kampuni ya simu husika (hakuitaja) kwa vile ‘Centre
Number’ iliyotumika kutuma ujumbe huo mfupi wa maneno ni 44780200332,
ambayo siyo ya mtandao wa kampuni husika bali ni ya mtandao ulio nje ya
nchi.
Alisema uchunguzi zaidi unaendelea kubaini chanzo cha ujumbe huo mfupi
wa simu na mtu aliyehusika kutuma kuutuma ili hatua za kisheria ziweze
kuchukua mkondo wake.
Mvutano wa madai ya ujumbe huo wa simu kati ya Mulongo na Lema ulizuka
mwishoni mwa Aprili mwaka huu, baada kutokea vurugu za wanafunzi wa Chuo
cha Uhasibu Arusha, hali ambayo ilipelekea kufunguwa kwa muda chuo
hicho.
Kabla ya kutokea kwa vurugu hizo, wanafunzi walikuwa wamesitisha masomo
wakitaka kuandamana hadi kwa mkuu wa mkoa kulalamikia kuuawa kwa
mwanafunzi mwenzao aliyechomwa kisu na watu wasiojulikana.
Lema alidaiwa na Mulongo kwamba alihusika kuwachochea wanafunzi ambao
baadaye walimzomea mkuu wa mkoa wakati alipotaka kuzungumza nao.
Hali hiyo ilisababisha kuzuka kwa vurugu iliyopelekea polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kutumia mabomu ya machozi.
Baada ya hapo Mulongo aliamrisha kukamatwa kwa Lema au la alitakiwa ajisalimishe, suala ambalo halifanyika.
Lema alimtumu Mulongo kwa amri hiyo akielezea kuwa huo ni mwendelezo wa
manyanyaso anayofanyiwa na mkuu huyo wa mkoa na akadai kuwa ametumiwa
ujumbe huo na mkuu wa mkoa.
BY JOHN NGUNGE
SOURCE: NIPASHE
0 comments:
Post a Comment