MLIE TUU ! WASTARA HATAOLEWA BONGO TENA


Na Imelda Mtema
KAKA wa staa wa Filamu za Kibongo, Wastara Juma aitwaye Juma Juma ameliambia Risasi Mchanganyiko kwamba dada yake hatafunga  tena ndoa nyingine hapa nchini.

“Iwapo dada yangu akitaka kuolewa atafanya hivyo Uarabuni siyo hapa kabisa,” alisema kaka huyo na kudai kuwa ameshuhudia mateso mengi ya dada yake kwa wanaume wa Kitanzania.

Kaka huyo amesisitiza kwamba wanaume wasipate tabu ya kumuuliza dada yake kuhusu suala la ndoa kwani watajisumbua bure.
Juma alizungumza kwa niaba ya dada yake ambaye awali alipigiwa simu ili kuulizwa kama alikuwa na mpango wa kufunga ndoa nyingine hapa nchini.

Hata hivyo, Wastara alimwachia kaka yake huyo kujibu badala yake, ingawaje kaka huyo hakufafanua kama dada yake ameshapata mtu wa kufunga naye ndoa huko Uarabuni.

Wastara alifunga ndoa tatu na wanaume tofauti na mume wake wa mwisho alikuwa msanii wa filamu, Juma Juma Kilowoko ‘Sajuki’ aliyefariki dunia mapema mwaka huu.

Source:Global Publishers

Na Imelda Mtema
KAKA wa staa wa Filamu za Kibongo, Wastara Juma aitwaye Juma Juma ameliambia Risasi Mchanganyiko kwamba dada yake hatafunga  tena ndoa nyingine hapa nchini.

“Iwapo dada yangu akitaka kuolewa atafanya hivyo Uarabuni siyo hapa kabisa,” alisema kaka huyo na kudai kuwa ameshuhudia mateso mengi ya dada yake kwa wanaume wa Kitanzania.

Kaka huyo amesisitiza kwamba wanaume wasipate tabu ya kumuuliza dada yake kuhusu suala la ndoa kwani watajisumbua bure.
Juma alizungumza kwa niaba ya dada yake ambaye awali alipigiwa simu ili kuulizwa kama alikuwa na mpango wa kufunga ndoa nyingine hapa nchini.

Hata hivyo, Wastara alimwachia kaka yake huyo kujibu badala yake, ingawaje kaka huyo hakufafanua kama dada yake ameshapata mtu wa kufunga naye ndoa huko Uarabuni.

Wastara alifunga ndoa tatu na wanaume tofauti na mume wake wa mwisho alikuwa msanii wa filamu, Juma Juma Kilowoko ‘Sajuki’ aliyefariki dunia mapema mwaka huu.

Source:Global Publishers

BILIONEA WA HOME SHOPPING CENTRE ASHINDIKANA KUTIBIWA

Hakika aliyemmwagia tindikali bilionea Said Mohamed Saad, alifanya kitendo kibaya kupitiliza, kwani athari ambazo amemsababishia ni kubwa kiasi ambacho hata upatikanaji wa tiba mahsusi umekuwa wa kutangatanga. 
Gazeti hili linazo taarifa za ndani na zenye uhakika kuwa Said ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Home Shopping Centre, amekimbizwa Ujerumani kwa matibabu zaidi baada ya kushindikana Afrika Kusini alikopelekwa awali.
Said alimwagiwa tindikali Julai 19, mwaka huu, mishale ya saa 2 usiku akiwa kwenye moja ya maduka yake yaliyopo kwenye jengo analodaiwa kulimiliki la Msasani Mall.
Ilielezwa kuwa baada ya kumwagiwa tindikali, alikimbizwa kwenye Hospitali ya Ami Wellness Centre iliyopo Masaki, Dar es Salaam lakini ndani ya kipindi kisichozidi dakika 60, alichukuliwa na kupandishwa ndege kupelekwa Afrika Kusini.
AFRIKA KUSINI MATUMAINI KIDOGO
Ndugu wa Said aliyeomba hifadhi ya jina lake gazetini, alisema kuwa akiwa Afrika Kusini, ilionekana kwamba bilionea huyo anatakiwa kufanyiwa oparesheni ya uso ili kuondoa ngozi iliyoathiriwa na tindikali, vilevile kulifanyia jicho upasuaji.
“Sehemu ya usoni kushuka kifuani upande wa kulia na mkono wenyewe wa kulia ndiyo maeneo katika mwili wa ndugu yetu yaliyoathirika zaidi na tindikali,” alisema ndugu huyo wa ndani kabisa kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza:
“Jicho la kulia lenyewe limepata athari kidogo, kwani inaonekana wakati mmwagaji akifanya kile kitendo, yeye alifumba macho kwa hiyo tindikali haikuingia ndani ya jicho, iliishia kwa juu.
“Ila kwa vile tindikali ilimwagika kwa wingi juu kwenye jicho la kulia na kutokana na ukali wa tindikali aliyomwagiwa, imesababisha kutengenezwa kwa mtoto wa jicho kwa hiyo hawezi kuona mbali.
“Uamuzi wa kumpeleka Ujerumani uliafikiwa baada ya kujiridhisha kwamba kule kuna wataalamu kuliko Afrika Kusini. Oparesheni ya uso kubadili ngozi iliyoathirika, vilevile kufanya upasuaji wa jicho na kuliweka sawa ni mambo ambayo tulijiridhisha yanawezekana Ujerumani.”
AKATAA KUTAJA JINA LA HOSPITALI
Kwa mujibu wa ndugu huyo, Said aliondolewa Afrika Kusini na kupelekwa Ujerumani, Agosti 3, mwaka huu na tangu hapo taarifa zake zimefanywa siri kubwa ili kulinda usalama wake.
“Hata wakati nazungumza na wewe kama mwandishi wa habari, nilijua tu lazima utaniuliza kuhusu jina la hospitali aliyolazwa Ujerumani. Ukweli ni kwamba siwezi kukwambia. Tunafanya hivyo kwa ajili ya usalama wa ndugu yetu.
“Tukio la kumwagiwa tindikali ni zito sana, imeshajionesha wazi namna ambavyo kuna watu hawampendi, hao maadui wakijua hospitali aliyolazwa, wanaweza kufanya juu chini wamfikie na kumdhuru kwa mara nyingine. Hilo jambo hatutaki kabisa litokee,” alisema ndugu huyo.
NDUGU, WATOTO WAKE WAZUIWA KWENDA UJERUMANI
Habari zaidi zinabainisha kuwa ndugu wa Said walipanga kwenda Ujerumani kumtembelea lakini walizuiwa kwa sababu awamu hii, viongozi wa familia yake wamezingatia usiri.
“Kuna watoto wake walikwenda Afrika Kusini na walikuwepo wakati anasafirishwa kwenda Ujerumani lakini waliambiwa warudi Tanzania kwa sababu kule Ujerumani utaratibu umebadilika. Watu wachache wanaohusika na huduma pamoja na usalama wake ndiyo pekee wanaoruhusiwa,” alisema, akaongeza:
“Wapo ndugu wengine kutoka Saudi Arabia na Oman, vilevile nao wamezuiwa kwenda Ujerumani kumwona. Ni katika kuhakikisha mambo hayawi kama ilivyokuwa Afrika Kusini, maana kule ilishakuwa hatari, ndugu wengine wanaingia wodini, wanampiga picha na kusambaza mitandaoni. Safari hii mambo hayo hayatakiwi.”
APELEKWA UJERUMANI BAADA YA JK
Imeelezwa kwamba Said alipelekwa Ujerumani wiki moja baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete kwenda kumtembelea alipokuwa amelazwa kwenye hospitali moja nchini Afrika Kusini.
Dk. Kikwete, alikuwa kwenye ziara ya kikazi nchini Afrika Kusini alipokwenda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini ya Afrika (SADC), kuhusu pande tatu za umoja huo (Troika of SADC), hivyo kupata fursa ya kwenda kumjulia hali.
MUNGU AMPONYE SAID
Dawati la gazeti hili linamuombea Said apone kwani alionesha moyo wa ukarimu kwa familia 655 zilizokumbwa na mafuriko eneo la Jangwani, Desemba, 2011 kisha kuhamishiwa Mabwepande, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam.
MTUHUMIWA BADO KUKAMATWA
Kwa mujibu wa Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, Dar es Salaam, ACP Camillius Wambura alisema kwamba jeshi la polisi linaendelea kufanya kazi kwa nguvu na umakini mkubwa lakini mpaka sasa halijafanikiwa kumpata mtuhumiwa.
Hakika aliyemmwagia tindikali bilionea Said Mohamed Saad, alifanya kitendo kibaya kupitiliza, kwani athari ambazo amemsababishia ni kubwa kiasi ambacho hata upatikanaji wa tiba mahsusi umekuwa wa kutangatanga. 
Gazeti hili linazo taarifa za ndani na zenye uhakika kuwa Said ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Home Shopping Centre, amekimbizwa Ujerumani kwa matibabu zaidi baada ya kushindikana Afrika Kusini alikopelekwa awali.
Said alimwagiwa tindikali Julai 19, mwaka huu, mishale ya saa 2 usiku akiwa kwenye moja ya maduka yake yaliyopo kwenye jengo analodaiwa kulimiliki la Msasani Mall.
Ilielezwa kuwa baada ya kumwagiwa tindikali, alikimbizwa kwenye Hospitali ya Ami Wellness Centre iliyopo Masaki, Dar es Salaam lakini ndani ya kipindi kisichozidi dakika 60, alichukuliwa na kupandishwa ndege kupelekwa Afrika Kusini.
AFRIKA KUSINI MATUMAINI KIDOGO
Ndugu wa Said aliyeomba hifadhi ya jina lake gazetini, alisema kuwa akiwa Afrika Kusini, ilionekana kwamba bilionea huyo anatakiwa kufanyiwa oparesheni ya uso ili kuondoa ngozi iliyoathiriwa na tindikali, vilevile kulifanyia jicho upasuaji.
“Sehemu ya usoni kushuka kifuani upande wa kulia na mkono wenyewe wa kulia ndiyo maeneo katika mwili wa ndugu yetu yaliyoathirika zaidi na tindikali,” alisema ndugu huyo wa ndani kabisa kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza:
“Jicho la kulia lenyewe limepata athari kidogo, kwani inaonekana wakati mmwagaji akifanya kile kitendo, yeye alifumba macho kwa hiyo tindikali haikuingia ndani ya jicho, iliishia kwa juu.
“Ila kwa vile tindikali ilimwagika kwa wingi juu kwenye jicho la kulia na kutokana na ukali wa tindikali aliyomwagiwa, imesababisha kutengenezwa kwa mtoto wa jicho kwa hiyo hawezi kuona mbali.
“Uamuzi wa kumpeleka Ujerumani uliafikiwa baada ya kujiridhisha kwamba kule kuna wataalamu kuliko Afrika Kusini. Oparesheni ya uso kubadili ngozi iliyoathirika, vilevile kufanya upasuaji wa jicho na kuliweka sawa ni mambo ambayo tulijiridhisha yanawezekana Ujerumani.”
AKATAA KUTAJA JINA LA HOSPITALI
Kwa mujibu wa ndugu huyo, Said aliondolewa Afrika Kusini na kupelekwa Ujerumani, Agosti 3, mwaka huu na tangu hapo taarifa zake zimefanywa siri kubwa ili kulinda usalama wake.
“Hata wakati nazungumza na wewe kama mwandishi wa habari, nilijua tu lazima utaniuliza kuhusu jina la hospitali aliyolazwa Ujerumani. Ukweli ni kwamba siwezi kukwambia. Tunafanya hivyo kwa ajili ya usalama wa ndugu yetu.
“Tukio la kumwagiwa tindikali ni zito sana, imeshajionesha wazi namna ambavyo kuna watu hawampendi, hao maadui wakijua hospitali aliyolazwa, wanaweza kufanya juu chini wamfikie na kumdhuru kwa mara nyingine. Hilo jambo hatutaki kabisa litokee,” alisema ndugu huyo.
NDUGU, WATOTO WAKE WAZUIWA KWENDA UJERUMANI
Habari zaidi zinabainisha kuwa ndugu wa Said walipanga kwenda Ujerumani kumtembelea lakini walizuiwa kwa sababu awamu hii, viongozi wa familia yake wamezingatia usiri.
“Kuna watoto wake walikwenda Afrika Kusini na walikuwepo wakati anasafirishwa kwenda Ujerumani lakini waliambiwa warudi Tanzania kwa sababu kule Ujerumani utaratibu umebadilika. Watu wachache wanaohusika na huduma pamoja na usalama wake ndiyo pekee wanaoruhusiwa,” alisema, akaongeza:
“Wapo ndugu wengine kutoka Saudi Arabia na Oman, vilevile nao wamezuiwa kwenda Ujerumani kumwona. Ni katika kuhakikisha mambo hayawi kama ilivyokuwa Afrika Kusini, maana kule ilishakuwa hatari, ndugu wengine wanaingia wodini, wanampiga picha na kusambaza mitandaoni. Safari hii mambo hayo hayatakiwi.”
APELEKWA UJERUMANI BAADA YA JK
Imeelezwa kwamba Said alipelekwa Ujerumani wiki moja baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete kwenda kumtembelea alipokuwa amelazwa kwenye hospitali moja nchini Afrika Kusini.
Dk. Kikwete, alikuwa kwenye ziara ya kikazi nchini Afrika Kusini alipokwenda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini ya Afrika (SADC), kuhusu pande tatu za umoja huo (Troika of SADC), hivyo kupata fursa ya kwenda kumjulia hali.
MUNGU AMPONYE SAID
Dawati la gazeti hili linamuombea Said apone kwani alionesha moyo wa ukarimu kwa familia 655 zilizokumbwa na mafuriko eneo la Jangwani, Desemba, 2011 kisha kuhamishiwa Mabwepande, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam.
MTUHUMIWA BADO KUKAMATWA
Kwa mujibu wa Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, Dar es Salaam, ACP Camillius Wambura alisema kwamba jeshi la polisi linaendelea kufanya kazi kwa nguvu na umakini mkubwa lakini mpaka sasa halijafanikiwa kumpata mtuhumiwa.

'IDD AZZAN HAUZI UNGA'

WAKATI Jeshi la Polisi Tanzania likiweka bayana kwamba, linamchunguza Mbunge wa Kinondoni kwa ‘leseni’ ya CCM, Mheshimiwa Idd Mohamed Azzan kama kweli anajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, baadhi ya wapiga kura wake wameibuka na kuthubutu kusema kiongozi huyo hauzi unga.
Wakizungumza na Uwazi juzi Bamaga, Mwenge jijini Dar, wapiga kura hao kutokea CCM, walisema madai kwamba mbunge wao ni mfanyabiashara wa ‘unga’ yamewashangaza sana.
Walisema haiingii akilini hata kidogo kwa mtu ambaye amepata utajiri wake huku majirani wakimuona halafu aangushiwe kashfa ya kufanya biashara hiyo haramu.
“Sisi hapa (Magomeni Makanya) tunamjua Idd tangu zamani akiwa kijana mdogo. Alikuwa na teksi akiwa anaendesha mwenyewe, akaja akanunua ya pili.
“Mwaka 1986 aliziuza, akanunua daladala aina ya Costa, akawa anaendesha mwenyewe, tena ilikuwa inafanya safari za Pugu Kariakoo, akaja akanunua lori, akawa anaendesha mwenyewe,” alisema mzee Mussa, mkazi wa eneo hilo.
Naye Bakari au maarufu kwa jina la Jabu, alisema yeye anakumbuka mwaka 1986, mheshimiwa akiwa anasaka maisha alifanya biashara ya kupeleka redio Bujumbura nchini Burundi kisha anarudi na mashati yalikuwa maarufu kwa jina la Juliana, anauza Dar, tayari kipindi hicho Idd  ana fedha zake.
“Sasa leo wanapozuka watu na kusema anauza dawa za kulevya, tunashangaa sana. Sisi majirani zake achilia mbali kuwa wapiga kura wake tungejua.
“Watu wanaojazana nyumbani kwake kabla hajaamua kuikarabati hii nyumba hapa wengi ni wale wenye matatizo, wanaomba msaada,” alisema mzee huyo.
Mzee mwingine, Hussein alisema anakumbuka mwaka 1989, yeye alikuwa shahidi wakati Azzan alipokopeshwa semi trela aina ya Mercedes Benz na kaka yake kwa makubaliano ya kumlipa fedha mwaka 1992.
“Azzan alikubali masharti hayo, akawa anaendesha mwenyewe kwenda nje ya nchi. Alikuwa akienda Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi mpaka Kongo.
“Na alikuwa akirudi anatubebea zawadi za chakula wazee wake kwa sababu ya ukaribu, mwaka elfu moja mia tisa na tisini na mbili alilipa deni, semi trela ikawa yake na akanunua jingine kama hilo.
“Nakumbuka kuna mwaka alipata ajali mbaya sana kule Ngara, akaumia na kulazwa, tukapata taarifa.
“Alipotoka akaamua kuanzisha Kampuni ya Azzan Investment na kununua mabasi mengi ya kukodisha, ndivyo ninavyojua mimi asili ya utajiri wa huyu bwana. Azzan hauzi unga bwana,” alisema mzee huyo.
Siku hiyohiyo, Uwazi lilimtafuta kwa simu Mheshimiwa Azzan na kumuuliza kama anawajua wazee hao ambapo alisema ni wazee wake anaowaheshimu sana, lakini akaomba asiongee kwa undani sana kwa vile alikuwa kikaoni.
Hivi karibuni, mtu mmoja aliyedai yupo jela Hong Kong, China kwa ishu ya unga aliandika majina ya watu aliodai ndiyo wafanyabiashara wa madawa ya kulevya na kuyatumbukiza majina hayo mtandaoni. Miongoni mwa majina hayo limo la Idd Azzan.
WAKATI Jeshi la Polisi Tanzania likiweka bayana kwamba, linamchunguza Mbunge wa Kinondoni kwa ‘leseni’ ya CCM, Mheshimiwa Idd Mohamed Azzan kama kweli anajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, baadhi ya wapiga kura wake wameibuka na kuthubutu kusema kiongozi huyo hauzi unga.
Wakizungumza na Uwazi juzi Bamaga, Mwenge jijini Dar, wapiga kura hao kutokea CCM, walisema madai kwamba mbunge wao ni mfanyabiashara wa ‘unga’ yamewashangaza sana.
Walisema haiingii akilini hata kidogo kwa mtu ambaye amepata utajiri wake huku majirani wakimuona halafu aangushiwe kashfa ya kufanya biashara hiyo haramu.
“Sisi hapa (Magomeni Makanya) tunamjua Idd tangu zamani akiwa kijana mdogo. Alikuwa na teksi akiwa anaendesha mwenyewe, akaja akanunua ya pili.
“Mwaka 1986 aliziuza, akanunua daladala aina ya Costa, akawa anaendesha mwenyewe, tena ilikuwa inafanya safari za Pugu Kariakoo, akaja akanunua lori, akawa anaendesha mwenyewe,” alisema mzee Mussa, mkazi wa eneo hilo.
Naye Bakari au maarufu kwa jina la Jabu, alisema yeye anakumbuka mwaka 1986, mheshimiwa akiwa anasaka maisha alifanya biashara ya kupeleka redio Bujumbura nchini Burundi kisha anarudi na mashati yalikuwa maarufu kwa jina la Juliana, anauza Dar, tayari kipindi hicho Idd  ana fedha zake.
“Sasa leo wanapozuka watu na kusema anauza dawa za kulevya, tunashangaa sana. Sisi majirani zake achilia mbali kuwa wapiga kura wake tungejua.
“Watu wanaojazana nyumbani kwake kabla hajaamua kuikarabati hii nyumba hapa wengi ni wale wenye matatizo, wanaomba msaada,” alisema mzee huyo.
Mzee mwingine, Hussein alisema anakumbuka mwaka 1989, yeye alikuwa shahidi wakati Azzan alipokopeshwa semi trela aina ya Mercedes Benz na kaka yake kwa makubaliano ya kumlipa fedha mwaka 1992.
“Azzan alikubali masharti hayo, akawa anaendesha mwenyewe kwenda nje ya nchi. Alikuwa akienda Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi mpaka Kongo.
“Na alikuwa akirudi anatubebea zawadi za chakula wazee wake kwa sababu ya ukaribu, mwaka elfu moja mia tisa na tisini na mbili alilipa deni, semi trela ikawa yake na akanunua jingine kama hilo.
“Nakumbuka kuna mwaka alipata ajali mbaya sana kule Ngara, akaumia na kulazwa, tukapata taarifa.
“Alipotoka akaamua kuanzisha Kampuni ya Azzan Investment na kununua mabasi mengi ya kukodisha, ndivyo ninavyojua mimi asili ya utajiri wa huyu bwana. Azzan hauzi unga bwana,” alisema mzee huyo.
Siku hiyohiyo, Uwazi lilimtafuta kwa simu Mheshimiwa Azzan na kumuuliza kama anawajua wazee hao ambapo alisema ni wazee wake anaowaheshimu sana, lakini akaomba asiongee kwa undani sana kwa vile alikuwa kikaoni.
Hivi karibuni, mtu mmoja aliyedai yupo jela Hong Kong, China kwa ishu ya unga aliandika majina ya watu aliodai ndiyo wafanyabiashara wa madawa ya kulevya na kuyatumbukiza majina hayo mtandaoni. Miongoni mwa majina hayo limo la Idd Azzan.

LIYUMBA AKWAA BALAA JIPYA,YEYE NA MKEWE HAPATOSHI

MNAMKUMBUKA aliyekuwa kigogo wa Benki Kuu ya Tanzania aliyefungwa jela miaka miwili kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na ufujaji wa mali za umma, Amatus Joackim Liyumba? Basi amekwaa balaa jipya, Uwazi linajua kila kitu
Liyumba na mwanamke aliyedai ni mke wake, Aurelia Paulo Ngowi wamefikishana Mahakama ya Kinondoni, Dar kisa kikidaiwa ni mzee huyo kumtaka mwanamke huyo kuondoka haraka kwenye nyumba anayoishi na watoto wao wawili.
Nyumba hiyo ipo Mbezi ya Afrikana, jijini Dar. Mbali na kuwa makazi, lakini sehemu ya mbele ya nyumba hiyo ni Hoteli Amjen yenye kupata wateja kila siku.
Jina la Amjen linadaiwa ni muuganiko wa majina ya Amatus na Jennifer ambaye ni mtoto mmoja kati ya hao wawili wa mzee huyo. 
Aurelia ndiye aliyekimbilia mahakamani kuomba msaada ambapo shauri lake lilifunguliwa kwa namba 59, 2013 mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Rugemalira.
Baada ya ombi hilo, mahakama ilimwamuru Liyumba kumwacha mkewe na watoto hao waendelee kuishi kwenye nyumba hiyo mpaka shauri hilo litakapotatuliwa kisheria.
Haikujulikana mara moja kama Liyumba anataka mkewe na watoto waondoke kwenye nyumba hiyo na yeye kwa sasa anaishi wapi. 
Jitihada za kumtafuta zilifanyika, simu yake ya mkononi haikuwa hewani huku ikidaiwa kwamba namba husika haitumii tena.
Baadhi ya watu wake wa karibu waliliambia Uwazi kwamba, kwa sasa Liyumba anaishi Kinondoni, Dar es Salaam lakini kupatikana kwenye simu ni ishu nyingine.

MNAMKUMBUKA aliyekuwa kigogo wa Benki Kuu ya Tanzania aliyefungwa jela miaka miwili kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na ufujaji wa mali za umma, Amatus Joackim Liyumba? Basi amekwaa balaa jipya, Uwazi linajua kila kitu
Liyumba na mwanamke aliyedai ni mke wake, Aurelia Paulo Ngowi wamefikishana Mahakama ya Kinondoni, Dar kisa kikidaiwa ni mzee huyo kumtaka mwanamke huyo kuondoka haraka kwenye nyumba anayoishi na watoto wao wawili.
Nyumba hiyo ipo Mbezi ya Afrikana, jijini Dar. Mbali na kuwa makazi, lakini sehemu ya mbele ya nyumba hiyo ni Hoteli Amjen yenye kupata wateja kila siku.
Jina la Amjen linadaiwa ni muuganiko wa majina ya Amatus na Jennifer ambaye ni mtoto mmoja kati ya hao wawili wa mzee huyo. 
Aurelia ndiye aliyekimbilia mahakamani kuomba msaada ambapo shauri lake lilifunguliwa kwa namba 59, 2013 mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Rugemalira.
Baada ya ombi hilo, mahakama ilimwamuru Liyumba kumwacha mkewe na watoto hao waendelee kuishi kwenye nyumba hiyo mpaka shauri hilo litakapotatuliwa kisheria.
Haikujulikana mara moja kama Liyumba anataka mkewe na watoto waondoke kwenye nyumba hiyo na yeye kwa sasa anaishi wapi. 
Jitihada za kumtafuta zilifanyika, simu yake ya mkononi haikuwa hewani huku ikidaiwa kwamba namba husika haitumii tena.
Baadhi ya watu wake wa karibu waliliambia Uwazi kwamba, kwa sasa Liyumba anaishi Kinondoni, Dar es Salaam lakini kupatikana kwenye simu ni ishu nyingine.

SERIKALI YAKANUSHA KUWA MAMA SALMA KIKWETE SI MNYARWANDA NA WALA KIKWETE SI SHEMEJI YAO


Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Assah Mwambene leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara hiyo amekanusha taarifa zilizoandikwa kwenye mtandao wa “twitter ”  na  wanyarwanda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni shemeji wa aliyekuwa Rais wa Rwanda Juvenal Havyarimana. 

“Taarifa hizi haina ukweli wowote na zinalenga kumpaka matope Rais Jakaya Mrisho Kikwete,” amesema Mwambene na kufafanua kuwa lengo la mitandao ya kijamii ni kuhabarisha na kuelimisha umma wala siyo kupotosha jamii kwa kuandika habari zisizo na ukweli wowote.

Madai  hayo  yaliandikwa  jana  na  mitandao  ya  Rwanda  wakidai  kuwa  mama  Salma  Kikwete  ni  Mnyarwanda  na  ni  binamu  wa  aliyekuwa  rais  wa  zamani  wa  Rwanda.



Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Assah Mwambene leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara hiyo amekanusha taarifa zilizoandikwa kwenye mtandao wa “twitter ”  na  wanyarwanda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni shemeji wa aliyekuwa Rais wa Rwanda Juvenal Havyarimana. 

“Taarifa hizi haina ukweli wowote na zinalenga kumpaka matope Rais Jakaya Mrisho Kikwete,” amesema Mwambene na kufafanua kuwa lengo la mitandao ya kijamii ni kuhabarisha na kuelimisha umma wala siyo kupotosha jamii kwa kuandika habari zisizo na ukweli wowote.

Madai  hayo  yaliandikwa  jana  na  mitandao  ya  Rwanda  wakidai  kuwa  mama  Salma  Kikwete  ni  Mnyarwanda  na  ni  binamu  wa  aliyekuwa  rais  wa  zamani  wa  Rwanda.


ABIRIA 60 WANUSURIKA KUFA BAADA YA BASI LA TURU KUCHOMWA MOTO NA WANAKIJIJI HUKO SINGIDA.

Abiria wapatao 60 waliokuwa wanasafiri na basi la Turu linalofanya safari zake kati ya mkoa wa Singida na Haidom mkoani Manyara, wamelazimishwa kuteremka toka ndani ya basi hilo na wananchi zaidi ya mia mbili ( 200 ) wa vijiji vitatu, na kisha kulichoma moto basi hilo.


Taarifa toka eneo la tukio zinasema wananchi hao ni wa vijiji vya Singa, Idabagadu na Nkungi mkoani Singida, ambao baada ya kuhakikisha abiria wote wameshuka, walilichoma moto basi hilo ambalo limetekea sehemu kubwa.


Sababu ya wananchi hao kuchukua uamuzi huo ni kutokana na basi hilo kumgonga mwanakijiji mmoja na kufa wiki tatu zilizopita
Abiria wapatao 60 waliokuwa wanasafiri na basi la Turu linalofanya safari zake kati ya mkoa wa Singida na Haidom mkoani Manyara, wamelazimishwa kuteremka toka ndani ya basi hilo na wananchi zaidi ya mia mbili ( 200 ) wa vijiji vitatu, na kisha kulichoma moto basi hilo.


Taarifa toka eneo la tukio zinasema wananchi hao ni wa vijiji vya Singa, Idabagadu na Nkungi mkoani Singida, ambao baada ya kuhakikisha abiria wote wameshuka, walilichoma moto basi hilo ambalo limetekea sehemu kubwa.


Sababu ya wananchi hao kuchukua uamuzi huo ni kutokana na basi hilo kumgonga mwanakijiji mmoja na kufa wiki tatu zilizopita

HUNITAKI TENA KWA SABABU UMEPATA MWINGINE SASA KWA NINI UNANIVUA NGUO KWA MARAFIKI ZAKO?



Mimi ni Msichana wa Miaka 25 imetokea bahati mbaya tumeachana na Mchumba wangu baada ya yeye kupata msichana mwingine nimelia sana ili turudiane lakini wapi , kibaya zaidi akiwa na marafiki zake ananiongelea mimi kuwa eti sijui mapenzi ya kitandani kuwa eti huwa tukifanya nalala kama mgomba ...na mengine mengi ya siri ambayo labda ni kweli ama si kweli ....Sasa nashindwa kuelewa kwanini anivue nguo mbele ya rafiki zake baada ya kuachana ....naona aibu hata kupita mtaaani anaongea sana jamani ...Nifanyaje?


Mimi ni Msichana wa Miaka 25 imetokea bahati mbaya tumeachana na Mchumba wangu baada ya yeye kupata msichana mwingine nimelia sana ili turudiane lakini wapi , kibaya zaidi akiwa na marafiki zake ananiongelea mimi kuwa eti sijui mapenzi ya kitandani kuwa eti huwa tukifanya nalala kama mgomba ...na mengine mengi ya siri ambayo labda ni kweli ama si kweli ....Sasa nashindwa kuelewa kwanini anivue nguo mbele ya rafiki zake baada ya kuachana ....naona aibu hata kupita mtaaani anaongea sana jamani ...Nifanyaje?

Obama's Visit to Tanzania




 President Obama giving a show on the traditional dance performing at the Airport during his arrival to Tanzania JKIA.
 Walking with lots of happiness soon after his arrival Barak Obama with his host President Jakaya Mrisho Kikwete.
President Obama having a unique view of the Maasai traditional Morani dance.
Mr. Obama on the Tanzanian special Parade Guard at the JKIA
Presidents Obama and Kiwete with the first ladies waving across to the people of Tanzania
 This is how it was along the State House Avenue inside the main entrance.



 President Obama giving a show on the traditional dance performing at the Airport during his arrival to Tanzania JKIA.
 Walking with lots of happiness soon after his arrival Barak Obama with his host President Jakaya Mrisho Kikwete.
President Obama having a unique view of the Maasai traditional Morani dance.
Mr. Obama on the Tanzanian special Parade Guard at the JKIA
Presidents Obama and Kiwete with the first ladies waving across to the people of Tanzania
 This is how it was along the State House Avenue inside the main entrance.

A warm welcome by Senegal's President Macky Sall and his wife Marieme Faye Sall to President Obama and Mrs Obama

Obama, Senegal, President Sall, Dakar,President Barack Obama and his wife Michelle Obama shake hands with Senegal's President Macky Sall and his wife Marieme Faye Sall at the at the presidential palace in Dakar.
Obama, Senegal, President Sall, Dakar,President Barack Obama and his wife Michelle Obama shake hands with Senegal's President Macky Sall and his wife Marieme Faye Sall at the at the presidential palace in Dakar.

Barack and Michelle Obama look out from the Door of No Return while touring the House of Slaves in Senegal

Obama begins his Africa tourBarack and Michelle Obama look out from the Door of No Return while touring the House of Slaves, or Maison des Esclaves, at Goree Island off the coast of Dakar. Obama and his family toured the museum at the site where African slaves were held before going through the door and being shipped off the continent as slaves.
Obama begins his Africa tourBarack and Michelle Obama look out from the Door of No Return while touring the House of Slaves, or Maison des Esclaves, at Goree Island off the coast of Dakar. Obama and his family toured the museum at the site where African slaves were held before going through the door and being shipped off the continent as slaves.

Obama begins his Africa tour

Obama, Senegal, President Sall, Dakar,US President Barack Obama holds a joint press conference with his Senegalese counterpart President Macky Sall in Dakar. The visit marks the first day of Obama's Africa tour that will include visits to South Africa and Tanzania in addition to his three days in Senegal in order to emphasize human rights, youth engagement, and American trade and investment opportunities in the region.
Obama, Senegal, President Sall, Dakar,US President Barack Obama holds a joint press conference with his Senegalese counterpart President Macky Sall in Dakar. The visit marks the first day of Obama's Africa tour that will include visits to South Africa and Tanzania in addition to his three days in Senegal in order to emphasize human rights, youth engagement, and American trade and investment opportunities in the region.

Top 10 cities for car thefts

U.S. cities with the most car theft (Thinkstock)
In 1964, California crooners the Beach Boys sang about having "fun, fun, fun, 'til her daddy takes the T-bird away." Well, nearly 50 years later, Golden State residents still have to worry about someone snatching their ride from them — but it's not their daddy. The Des Plaines, Ill.-based National Insurance Crime Bureau has released its "Hot Spots" vehicle-theft report for 2012, and California once again dominates as a "hotbed for hot cars."

Of the top 10 hot spots for per-capita vehicle theft, California lays claim to eight, and the state of Washington to the balance. The NICB's list reviews vehicle thefts from the nation's metropolitan statistical areas; its data mirrors preliminary FBI vehicle-theft data for the same period. While there's nothing new in West Coast domination of the list, this year is special in that the 1.3% spike is the first annual increase following an eight-year downward trend in the crime, the NICB reported. The FBI will publish its final numbers in the fall.

The designated West region — composed of Alaska, Arizona, California, Colorado, Hawaii, Idaho, Montana, Nevada, New Mexico, Oregon, Utah, Washington and Wyoming — in 2012 experienced a 10.6% increase in vehicle thefts compared with 2011, bringing the entire nation's average up despite declines elsewhere. The Midwest, Northeast and South reported reductions of 3.1%, 7.9% and 2.9%, respectively.

Last year's second-place finisher, Modesto, Calif., wrested control of the No. 1 spot from Fresno, Calif., knocking it down one spot; Modesto had 4,260 thefts for a rate of 816.52 per 100,000 population, while Fresno had 7,563 thefts but a lower rate of 797.87 due to its greater population. Newcomers to this year's list are the San Jose-Sunnyvale-Santa Clara, Calif., area at No. 7, up from No. 20 last year, as well as Redding, Calif., all the way up to No. 10 from No. 40 in 2011. The Midland, Mich., and Kahului-Wailuku-Lahaina, Hawaii, areas boasted the fewest car thefts, with fewer than 20 each and a rate of less than 22.

The NICB advises motorists to take precautions against vehicle theft starting with common-sense measures like removing keys from the ignition, locking doors and closing windows, and parking in well-lit areas. Beyond that, bigger and better anti-theft measures include installing a warning device such as a car alarm, using immobilizing devices such as a smart key or fuse cutoffs and using a tracking device that emits a signal to authorities if the vehicle is stolen.
U.S. cities with the most car theft (Thinkstock)
In 1964, California crooners the Beach Boys sang about having "fun, fun, fun, 'til her daddy takes the T-bird away." Well, nearly 50 years later, Golden State residents still have to worry about someone snatching their ride from them — but it's not their daddy. The Des Plaines, Ill.-based National Insurance Crime Bureau has released its "Hot Spots" vehicle-theft report for 2012, and California once again dominates as a "hotbed for hot cars."

Of the top 10 hot spots for per-capita vehicle theft, California lays claim to eight, and the state of Washington to the balance. The NICB's list reviews vehicle thefts from the nation's metropolitan statistical areas; its data mirrors preliminary FBI vehicle-theft data for the same period. While there's nothing new in West Coast domination of the list, this year is special in that the 1.3% spike is the first annual increase following an eight-year downward trend in the crime, the NICB reported. The FBI will publish its final numbers in the fall.

The designated West region — composed of Alaska, Arizona, California, Colorado, Hawaii, Idaho, Montana, Nevada, New Mexico, Oregon, Utah, Washington and Wyoming — in 2012 experienced a 10.6% increase in vehicle thefts compared with 2011, bringing the entire nation's average up despite declines elsewhere. The Midwest, Northeast and South reported reductions of 3.1%, 7.9% and 2.9%, respectively.

Last year's second-place finisher, Modesto, Calif., wrested control of the No. 1 spot from Fresno, Calif., knocking it down one spot; Modesto had 4,260 thefts for a rate of 816.52 per 100,000 population, while Fresno had 7,563 thefts but a lower rate of 797.87 due to its greater population. Newcomers to this year's list are the San Jose-Sunnyvale-Santa Clara, Calif., area at No. 7, up from No. 20 last year, as well as Redding, Calif., all the way up to No. 10 from No. 40 in 2011. The Midland, Mich., and Kahului-Wailuku-Lahaina, Hawaii, areas boasted the fewest car thefts, with fewer than 20 each and a rate of less than 22.

The NICB advises motorists to take precautions against vehicle theft starting with common-sense measures like removing keys from the ignition, locking doors and closing windows, and parking in well-lit areas. Beyond that, bigger and better anti-theft measures include installing a warning device such as a car alarm, using immobilizing devices such as a smart key or fuse cutoffs and using a tracking device that emits a signal to authorities if the vehicle is stolen.